Header Ads

Polisi wengine 5 wauawa katika shambulio Kenya



Maafisa wengine wane waliuawa katika eneo lililopo karibu na hilo siku ya Jumnatatu
NAIROBI, Kenya
MAOFISA watano wa polisi nchini, wameuawa baada ya gari lao kukanyaga bomu lililotegwa barabarani Kaskazini Mashariki mwa mji wa Liboi karibu na mpaka na Somalia.

Shambulio hilo lilitokea karibu na eneo lile lile, ambapo maofisa wengine wanne waliuawa katika shambulio jingine la bomu siku ya Jumatano ambalo kundi la Al-Shabab limekiri kulitekeleza.
Maofisa wengine watano waliuawa katika mashambulio tofauti ya mabomu siku ya Jumatatu katika kaunti Jirani ya Mandera.
Kundi la wapiganaji wa Al-Shabab, limefanya mashambulio kadhaa nchini katika siku za hivi karibuni. Kundi hilo lenye makao yake makuu Somalia, linaitaka Kenya kuondoa majeshi yake yanayohudumu chini ya vikosi vya AMISOM.
Mwandishi wa BBC, Mohammud Ali ameripoti kwamba shambulio hilo la Mandera lililenga gari la gavana wa kaunti hiyo, Ali Roba.
Roba alichapisha ujumbe katika ukurasa wake wa Facebook siku ya Jumatatu kwamba, alipoteza mlinzi wake katika shambulio hilo. Ni shambulio la tatu ambalo lilimlenga Roba katika kipindi cha siku tatu.

No comments

Powered by Blogger.