Header Ads

Polisi wamzuia kiongozi wa upinzani Afrika Kusini kuingia Zambia



Kiongozi wa Upinzani nchini Afrika kusini Mmusi Maimane
LUSAKA, Zambia
POLISI nchini, wamemzuia kiongozi wa chama kikuu cha upinzani cha Democratic Alliance (DA) cha Afrika Kusini, Mmusi Maimane kuingia nchini.

Maimane (pichani), alikuwa akitarajiwa kuhudhuria kesi inayomkabili kiongozi wa upinzani nchini, Hakainde Hichilema.
Hichilema anakabiliwa na mashtaka ya uhaini, baada ya kushindwa kutoa njia kwa msafara wa Rais Edgar Lungu, hali ambayo inadaiwa kuhatarisha maisha ya mkuu huyo wa nchi.
Kiongozi huyo wa upinzani nchini Afrika Kusini, amesema alilazimika kurudi nyumbani baada ya maofisa kuingia ndani ya ndege ya Shirika la ndege la Afrika Kusini aliyokuwa akisafiri nayo mjini Lusaka, kumvamia na kumnyang'anya simu yake.
Hata hivyo bado hakuna taarifa zozote zilizotolewa na Serikali ya Zambia.

No comments

Powered by Blogger.