FBI wamchunguza mkwe wa Trump, Kushner
Ripoti
zinasema kuwa wachunguzi wanaamini ana habari muhimu lakini sio mshukiwa wa
uhalifu. FBI linachunguza hatua ya Urusi kuingilia uchaguzi wa urais wa 2016
nchini na ushirikiano wa kundi la kampeni la Rais Trump.
Rais
Trump amekana madai yoyote ya kujihusisha na Urusi wakati wa kampeni. Wakili wa
Kushner amesema kuwa mteja wake atashirikiana na wachunguzi hao kuhusu
uchunguzi wowote.
Rais
Trump ametaja hali hiyo kuwa ‘uwindaji’ mkubwa wa kiongozi katika historia ya
Marekani.
Vitengo
vya ujasusi vinaamini Urusi ilijaribu kukisaidia chama cha Republican kushinda
uchaguzi huo, dhidi ya mgombea wa chama cha Democrat, Hillary Clinton.
Maofisa
wa Marekani ambao walikataa kutajwa, waliiambia chombo cha habari cha NBC
kwamba hatua ya kumchunguza Kushner mwenye umri wa miaka 36 haimaanishi kwamba
wachunguzi wanamshuku kuhusu uhalifu fulani na kwamba wanataka kumshtaki.
Kwingineko,
gazeti la Washington Post limeripoti kwamba wachunguzi hao walikuwa wakiangazia
mikutano aliyofanya mwaka uliopita na Balozi wa Urusi nchini, Sergei Kislyak na
mfanyakazi mmoja wa benki kutoka Moscow.
No comments