Header Ads

Njiwa adakwa akisafirisha dawa za kulevya Kuwait



Madawa hayo ya kulevya yalikuwa aina ya ketamine
KUWAIT CITY, Kuwait
MAOFISA wa forodha nchini, wamemkamata njiwa ambaye alikuwa amebeba dawa za kulevya katika mkoba mdogo mgongoni.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na gazeti la Al-Rai, njiwa huyo alipatikana na jumla ya tembe 178 ziliwekwa katika mfuko huo uliokuwa umepachikwa mgongoni mwake. Ndege huyo alinaswa karibu na jumba la forodha jijini Abdali, karibu na mpaka na Iraq.
Mwanahabari wa Al-Rai, alisema kuwa dawa hizo za kulevya zilikuwa aina ya Ketamine, nusukaputi ambayo pia hutumiwa kama dawa haramu katika sherehe.
Maafisa wa forodha wanaripotiwa kufuatilia njiwa huyo kabla ya kumshika
Abdullah Fahmi aliiambia BBC kwamba maofisa wa forodha walijua awali kuwa njiwa walikuwa wakitumiwa kusafirisha dawa za kulevya, lakini hii ilikuwa mara ya kwanza kwa ndege aina hiyo kunaswa katika harakati hizo.
Maofisa wa utekelezaji wa sheria katika nchi nyingine, wamewahi kuripoti visa vya njiwa waliodaiwa kutumiwa kusafirisha dawa za kulevya ya bei ghali japo kwa viwango vidogo.
Mwaka wa 2015, askari wa magereza nchini Costa Rica walimnasa njiwa aliyekuwa amebeba dawa za kulevya aina ya kokeni na bangi kwenye kipochi.
Na mwaka wa 2011, polisi wa Colombia walimkuta njiwa ambaye alishindwa kuruka juu ya ukuta mrefu wa jela kwa sababu ya uzito wa mzigo wa dawa za kulevya aina ya kokeni na bangi aliyopachikwa.
Njiwa wametumika kupeperusha ujumbe tangu enzi za Roma, wakitumia uwezo wao wa kurudi nyumbani walikotoka.


No comments

Powered by Blogger.