Header Ads

Polisi Uingereza walalamikia picha za mlipuko wa Manchester



Picha za shambulio zilizochapishwa na gazeti hilo
LONDON, Uingereza
POLISI nchini, wameyalaumu machapisho yaliyotolewa katika gazeti la New York Times la Marekani juu ya picha na taarifa kutoka katika eneo ambalo shambulio la bomu lilitokea mjini Manchester.

Maofisa wamesema kuvuja kwa picha hizo kunaharibu uchunguzi wa polisi na kuondoa imani na washirika wao katika masuala ya kiintelejinsia. Picha hizo zinaonesha vitu mbalimbali ambavyo vingetumika kama ushahidi, kama vile betri na vitu vingine vyenye muonekano wa vilipuzi.
Hata hivyo gazeti hilo la Marekani, limejitetea juu ya picha hizo ambazo imesema zinaashiria kuwa bomu lililotumika katika shambulio hilo kwa kiasi kikubwa linaonekana kuwa ni la kisasa.
Waziri Mkuu, Theresa May anatarajiwa kulipeleka suala hilo kwa Rais wa Marekani, Donald Trump wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa Jumuia ya NATO, ambao unafanyika leo.

No comments

Powered by Blogger.