Header Ads

Manchester United watwaa kombe la Europa



http://e0.365dm.com/17/05/16-9/20/skysports-europa-league_3962091.jpg?20170524220239
STOCKHOLM, Sweden
MANCHESTER United wamefanikiwa kuibuka washindi wa Kombe la Europa, baada ya kuifunga Ajax Amsterdam kwa mabao 2-0 katika fainali iliyochezwa uwanja wa Friends mjini hapa.

Magoli ya Paul Pogba na Henrick Mkhitaryan yameipa United sio tu Kombe la Europa, bali pia nafasi ya kucheza Klabu Bingwa Ulaya msimu ujao.
Mapema kabla ya mchezo huo kuanza, timu hizo mbili zilitoa heshima zao kwa watu waliopoteza maisha katika shambulio mjini Manchester. Pia wachezaji wa Manchester United na refa wa mchezo huo, walivaa vitambaa vyeusi mikononi kama ishara ya heshima kwa waathirika.
Image result for Man Utd victory yesterday in Europa 
Wafungaji wa mabao ya Man United, Henrick Mkhitaryan aliyefunga bao la pili (kushoto) na Paul Pogba (kulia) ambaye alifunga bao la kwanza wakishangilia bao la pili. Anayewakimbilia nyuma ni Chris Smalling

Wakicheza bila ya mfungaji bora wao Zlatan Ibrahimovic, pamoja na mabeki Marcos Rojo, na Luke Shaw, pamoja na Erick Bailly anayetumikia adhabu ya kadi nyekundu, kikosi cha Mourinho kililazimika kujituma kwenye mchezo huu wa 64 msimu huu.
Wakitumia uzoefu, pamoja na namna walivyojipanga, Man United waliweza kukisumbua kikosi cha Ajax ambacho kilikuwa na wachezaji chipukizi, wakiwa na wastani wa umri wa miaka 22.
Manchester United sasa wanaungana na Chelsea, Tottenahm na Manchester City katika kucheza Klabu Bingwa Ulaya. Pia ushindi huu utawaingizia kitita cha takriban pauni milioni 50.
Hili ni kombe la pili kwa Mourinho kushinda akiwa na United katika msimu wake wa kwanza. United walishinda Kombe la Ligi mwezi Februari mwaka huu.

No comments

Powered by Blogger.