Header Ads

Everton kufanya ziara Tanzania



Kampuni ya Sportpesa baada ya kuweka mkataba wa kuidhamini klabu ya Everton kutok Uingereza
LIVERPOOL, Uingereza
KLABU ya Everton, itazuru Tanzania kwa mechi za kirafiki kabla ya msimu wa 2017/18.

Kulingana na tovuti rasmi ya klabu hiyo, ziara hiyo ambayo ni ya kusheherekea udhamini mpya wa klabu hiyo na Sportpesa itakuwa na mechi ya kirafiki kati ya klabu hiyo na nyota wa Tanzania katika uwanja wa Taifa uliopo Dar Es salaam mnamo Julai 13, mwaka huu.
Everton itakuwa klabu ya kwanza ya Ligi Kuu ya Uingereza kucheza katika taifa hilo la Afrika Mashariki, na itakabliana dhidi ya mshindi wa kombe hilo la Sportpesa. Michuano hiyo utashirikisha timu kutoka Tanzania na Kenya ambazo zitatoa timu nne kila moja wao.
Mapema mwezi huu, Everton ilitangaza udhamini wa mamilioni ya fedha na Sportpesa ambapo jina la kampuni hiyo ya kamari litakuwa mbele ya tisheti za mabingwa hao wa zamani wa Uingereza kwa miaka mitano.
Tangu kuanzishwa kwake nchini Kenya mwaka 2014, kampuni hiyo imedhamini vilabu vingi, kuwekeza mbali na kushiriki katika kamari.

No comments

Powered by Blogger.