Header Ads

Naibu Waziri akagua ujenzi wa daraja la Kelema


Mhandisi Mshauri wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Mayamaya-Mela yenye urefu wa Kilometa 99.35, Leornado Licari akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani, kuhusu hatua za ujenzi zilizofikiwa za Daraja la Kelema Mita 220 linalounganisha wilaya ya Chemba na kondoa mkoani Dodoma, leo.


  


Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani (kushoto), akikagua hatua za ujenzi zilizofikiwa za Daraja la Kelema lenye urefu wa Meta 220 linalounganisha wilaya ya Chemba na kondoa mkoani Dodoma, leo. Kulia ni Mhandisi Mshauri wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Mayamaya-Mela Km 99.35, Mhandisi Leornado Licari.



Mkandarasi wa Kampuni ya Chicco, Li Jianzheng, akimwonesha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani (wa pili kulia), namna ya usukwaji nondo katika Daraja la Kelema lenye urefu wa meta 220 wakati alipokagua daraja hilo mkoani Dodoma leo.



Mhandisi Mshauri wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Mayamaya-Mela yenye urefu wa Kilometa 99.35, Leornado Licari akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani, kuhusu ujenzi wa Daraja la Msui lenye urefu wa mita 45 lililopo katika barabara hiyo, mkoani Dodoma, leo.



Mhandisi Mshauri wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Mela – Bonga yenye urefu wa Kilometa 88.8, Kini Kuyonza akimuonesha taarifa ya mradi Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani, wakati alipokuwa akikagua barabara hiyo, mkoani Manyara, leo.



Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani, akikagua zege lililowekwa katika barabara ya Mela-Bonga yenye urefu wa Kilometa 88.8 eneo la Mlima Kolo uliopo wilaya ya Kondoa, wakati alipokagua ujenzi wake, leo. Kulia ni Mhandisi Mshauri wa mradi huo, Mhandisi Kini Kuyonza.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani, amesema kuwa ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa daraja la Kelema lenye urefu wa mita 220 linalounganisha wilaya ya Chemba na Kondoa mkoani Dodoma.
Akizungumza leo mkoani Dodoma, mara baada ya kukagua daraja hilo lililopo katika barabara ya Mayamaya-Mela yenye urefu wa kilometa 99.35, Naibu Waziri huyo  alisema kuwa kukamilika kwa daraja hilo na  barabara za maingilio katika daraja hilo kutarahisisha  huduma ya usafiri kwa wananchi wa mkoa huo na mikoa jirani ya  Manyara na Arusha.
“Daraja hili na barabara zake ni kiungo muhimu kati ya mkoa huu na mikoa  ya Manyara na Arusha  na pia inaunganisha  nchi ya Tanzania, (Cape Town) South Afrika hadi (Cairo) Misri, hivyo kurahisisha huduma za  usafirishaji wa abiria na mizigo kutoka hapa kuelekea maeneo mengine,” alisema Ngonyani.
Aidha, Ngonyani aliitaka kampuni ya ujenzi ya Chico kuhakikisha inamaliza daraja hilo ifikapo mwezi wa kumi mwaka huu kama ilivyoandikwa kwenye mkataba ili wananchi kuweza kulitumia.
Kwa upande wake Mhandisi Mshauri wa mradi huo, Leornado Licari, alisema kwa sasa mradi umefikia asilimia 87 ambapo hivi karibuni wanatarajia kuweka lami.
“Nakuhakikishia kumaliza mradi huu kwa wakati kwani kazi zilizobaki kwa sasa hivi ni chache, kwa hiyo hadi kufikia mwezi Septemba tutakuwa tumeshakamilisha kazi zote,” alisema Licari.
Ngonyani yupo katika ziara ya kikazi ya siku moja katika mikoa ya Dodoma na Manyara ambapo pamoja na ukaguzi wa daraja hilo pia alikagua madaraja mengine matatu likiwemo la Msui, Kingali na Mela pamoja na ujenzi wa barabara ya Mela-Bonga yenye urefu wa kilometa 88.8.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano


No comments

Powered by Blogger.