Header Ads

Korea Kaskazini: Mazingira yakiruhsu tutazungumza na Marekani



http://cdn.images.express.co.uk/img/dynamic/78/590x/secondary/Choe-Son-Hui-is-expected-to-lead-the-North-Korean-delegation-835190.jpg
SEOUL, Korea Kusini
KOREA Kaskazini imesema kuwa itafanya mazungumzo na Marekani iwapo mazigira yataruhusu, kulingana na taarifa ambayo imeripotiwa na vyombo vya habari nchini.

Mjumbe Mwandamizi wa Korea Kaskazini, Choe Son Hui (pichani) alisema kuwa mazungumzo na Marekani yanawezekana kufuatia mkutano na waliokuwa maofisa wa Serikali ya Marekani nchini Norway.
Awali mwezi huu, Rais wa Marekani, Donald Trump alisema itakuwa heshima kubwa kukutana na Rais Kim Jong un. Matamshi yake yalijiri kufuatia ongezeko la hali ya wasiwasi kuhusu mipango ya Korea Kaskazini ya kinyuklia, pamoja na ile ya utengezaji wa makombora ya masafa marefu.
Hui ambaye ni ofisa katika Wizara ya Mambo ya Nje kuhusu masuala ya Marekani Kaskazini, alitoa kauli hiyo wakati alipokuwa akirudi Pyongyang baada ya mkutano mjini Oslo.

No comments

Powered by Blogger.