Header Ads

Video ya Boko Haram yaonesha wasichana waliokataa kuachiwa



http://cdn.24.co.za/files/Cms/General/d/4334/23e90c41787743ac9368c8db61b483ed.jpg
BORNO, Nigeria
KUNDI la wapiganaji wa Boko Haram, limetoa kanda ya video inayoonesha wasichana wanne waliokataa kurudi nyumbani ili kujiunga na familia zao.

Wiki iliyopita, wasichana 82 kati yao waliachiliwa huru baada ya miaka miwili wakiwa chini ya watekaji wao. Waliachiwa baada ya Serikali kuwaachia makamanda watano wa Boko Haram.
Kwa sasa, kuna wasichana takriban 100 wa Chibok ambao bado wanashikiliwa na wapiganaji hao huku Serikali ikisema kuwa mazungumzo ya kuwasihi Boko Haram kuwaachia huru yanaendelea.
Mmoja ya wasichana hao alionekana akibeba bunduki, huku mwingine akisema kuwa asingependelea kurudi nyumbani kwa sababu familia yake haiwezi kubadilika na kuwa Waislamu.
Wasichana 82 walioachiwa wiki iliyopita wanasubiri kuunganishwa na familia zao, lakini wataendelea kuwa chini ya uangalizi maalum wa Serikali.
Msemaji wa Ofisi ya Rais nchini, alisema kuwa msichana mwingine alitarajiwa kuachiliwa lakini akakataa. Inadaiwa kuwa wasichana wengine waliolewa na watekaji hao na kupata watoto.
BBC

No comments

Powered by Blogger.