Mashambulizi ya kompyuta kuathiri watu kuanzia kesho

Mdukuaji
LONDON,
Uingereza
WATAALAMU wa
usalama katika mitandao ya kompyuta, wameonya kwamba kunaweza kukatokea
mashambulio mengine sehemu mbalimbali za dunia, pale watu watakaporudi kazini
hapo leo.
Inakisiwa
kuwa kompyuta zaidi ya 120 katika nchi kama 100, zilidukuliwa mwishoni mwa wiki.
Lakini polisi wa Umoja wa Ulaya, wamesema walioathirika na udukuzi huo ni watu 200,000
katika mataifa 150.
Shambulio
hilo limeathiri watumiaji pamoja na ofisi za serikali, kampuni zinazotengeneza
magari, benki na huduma za afya. Shambulio hilo limezuia kompyuta kufikia takwimu,
na wanadai kikombozi, ili kuiachia kompyuta.
Uchambuzi
uliofanywa na BBC katika akaunti tatu za sarafu ya kidijitali, bitcoin,
unaonyesha washambuliaji wamelipwa kikombozi zaidi ya mara 100, jumla ya dola
karibu 30,000 (sh milioni 66).
No comments