Header Ads

Sarafu ya dhahabu yenye thamani kubwa yaibiwa Ujerumani

Vienna, Austria


Picha ya sarafu hiyo ya dhahabu iliyoibiwa. BBC



BERLIN, Ujerumani
SARAFU kubwa ambayo imetengenezwa kwa dhahabu, ikiwa na picha ya Malkia Elizabeth wa Uingereza, inayokadiriwa kuwa na thamani ya dola za Marekani milioni 4 (sh bilioni 8.8), imeibiwa kutoka kwenye makumbusho nchini.

Sarafu hiyo kutoka Canada imeandikwa kuwa ya thamani ya $1m, lakini kwa sababu imetengenezwa kwa kilo 100 za dhahabu, thamani yake ni ya juu kulingana na bei ya sasa ya dhahabu.
Iliibiwa usiku kutoka makavazi ya Bode mjini Berlin. Haijabainika ni vipi wezi walifanikiwa kuingia bila kugunduliwa na mtambo wa kuzuia wezi, na kisha kutoroka na sarafu hiyo ambayo nusu kipenyo chake ni cha nusu mita.
Wizi huo unaaminika kutekelezwa mwendo wa saa tisa unusu alfajiri ya jana Jumatatu. Sarafu hiyo inadaiwa kuwa nzito kiasi kwamba mtu mmoja hawezi kuibeba. Polisi wa eneo hilo wanasema huenda wezi hao waliingia kupitia dirisha.
Ngazi ilipatikana imetupwa kwenye reli iliyo karibu, msemaji wa polisi Winfrid Wenzel aliambia Reuters.
“Sarafu hiyo ilikuwa imehifadhiwa ndani ya sehemu isiyoweza kupenya risasi ndani ya makumbusho,” alisema.
Sarafu hiyo ilifuliwa mwaka 2007 na Royal Canadian Mint.

 

No comments

Powered by Blogger.