Canada kuhalalisha bangi mwakani
![https://files.merryjane.com/uploads/article/small_image/1250/MAKE_MARIJUANA_GROWING_A_GREENER_OPERATION_WIDE.jpg](https://files.merryjane.com/uploads/article/small_image/1250/MAKE_MARIJUANA_GROWING_A_GREENER_OPERATION_WIDE.jpg)
OTTAWA, Canada
MATUMIZI ya
bangi kwa kujiburudisha yatahalalishwa nchini, ifikapo tarehe mosi Julai 2018.
Serikali imeeleza
kuwa itawasilisha muswada wa kuhalalisha bangi ifikapo Aprili kwa mujibu wa
shirika la habari la Serikali la CBC.
Taarifa
ziliiambia CBC kuwa wanachama wa chama tawala cha Liberal hivi karibuni, walijulishwa
kuhusu muswada huo. CBC ilisema kuwa sheria hizo mpya zitaambatana na
mapendekezo yaliyotolewa na jopo lililoteuliwa na Serikali.
Baadhi
ya mapendekezo hayo ni kuwa, Canada itaruhusu kuuzwa kwa bangi kwa ajili ya
watu walio na zaidi ya umri wa zaidi ya miaka 18 kujiburudisha. Jopo kazi hilo,
pia lilipendekeza kuwa watu wazima wataruhusiwa kupanda hadi mimea minne ya
bangi na kumiliki hadi gramu 30 ya bangi iliyokaushwa.
Kwa mujibu
wa CBS, Serikali itasimamia kusambazwa kwa bangi na kuwapa leseni wazalishaji.
Ahadi wa Waziri
Mkuu, Justin Trudeau ya kuhalalisha bangi imechochea uvumi katika sekta hiyo.
Wazalishaji
kama kampuni ya Aphria, OrganiGram Holdings, na Canopy Growth, ambao ni
wazalishaji wakubwa zaidi wa bangi ya kutibu, yamekuwa vipnzi kwa wawekezaji wa
hisa.
No comments