Header Ads

Maneno ya kibaguzi yamponza raia wa Ujerumani



Lilongwe, Malawi
RAIA mmoja wa Ujerumani ambaye anafanya kazi nchini, Hinteregger Jurgen anakabiliwa na hati hati ya kurudishwa nchini kwao baada ya kudaiwa kutoa matamshi ya kibaguzi kwa mmoja wa wafanyakazi aliokuwa akiwasimamia.
Kwa mujibu wa gazeti la Nyasa Times, inadaiwa kuwa Jurgen alimwita ‘nyani’ dereva wake ambaye alikuwa akiendesha gari lililobeba maji baada ya kushindwa kulihimili na kugonga vizuizi na kupasuka tairi.

Msemaji wa Polisi nchini, Ignatius Easu alisema kuwa mara baada ya tukio hilo Jurgen ambaye anasimamia ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 47 aliteremka kwa hasira na kusikika akimwita ‘nyani’ dereva huyo kisha kumpokonya funguo za gari hilo.
Mara baada ya kukamatwa na polisi, Jurgen alipelekwa katika kituo cha polisi cha Songwe kilichopo mpakani mwa Malawi na Tanzania, ambapo aliwekwa mahabusu kabla ya kuletwa jijini hapa kwa ajili ya hatua nyinginezo.
Maneno hayo ya kibaguzi yaliyotolewa na msimamizi huyo, yalisababisha mgomo mkubwa wa wafanyakazi ambao walidai kuwa wanagoma kwa lengo la kumuunga mkono mfanyakazi mwenzao aliyedhalilishwa.

No comments

Powered by Blogger.