Header Ads

Daktari wa maradhi ya moyo Mtanzania apata tuzo

Nyagori

MOROGORO, Tanzania
DAKTARI Mshauri Mwandamizi wa magonjwa ya Moyo kutoka Hospitali ya Rufaa mkoani hapa, Dk Harun Emalda Nyagori (pichani) amepewa tuzo na Chuo Kikuu cha Magonjwa ya Moyo Marekani (American college of Cardiology).

Dk Nyagori ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Francis, amepewa tuzo ya kutambuliwa kwa utafiti na uzoefu wake katika ushauri kuhusu magonjwa ya moyo barani Afrika.
Baadhi ya utafiti uliofanywa na Dk Nyagori ni pamoja na kushindwa kufanya kazi kwa dawa za maradhi ya moyo nchini na changamoto za magonjwa ya moyo hapa nchini.
Tuzo nyingine alizopata ni kutoka kwa Jumuiya ya Madaktari Bingwa wa Maradhi ya Moyo barani Ulaya na Jumuiya ya Umoja wa Madaktari bingwa wa maradhi ya moyo nchini Mexico.
Dk Nyagori ni kati ya madaktari bingwa wachache nchini wanaoshauri na kutibu maradhi ya moyo yasiyohusiana na upasuaji. Amekuwa akifanya kazi hiyo kwa miaka saba sasa akiwasaidia wangonjwa katika mkoa wa Morogoro na mikoa jirani inayopakana na Morogoro.
Dk Nyagori pia aliwahi kupokea tuzo nyingine. Septemba 2015 alipokea tuzo kutoka Jumuiya ya Madaktari Bingwa wa Maradhi ya Moyo Barani Ulaya, London. Tuzo nyingine ni kutoka Jumuiya ya Umoja wa madaktari bingwa wa maradhi ya Moyo nchini Mexico mwaka 2016.
Kwa kushirikiana na madaktari wengine, Dk Nyagori amekuwa akiwatibu kwa wastani wagonjwa 40 hadi 60 kwa siku. Idadi inayofikia wastani wa wagonjwa 160 - 200 kwa wiki.


No comments

Powered by Blogger.