Header Ads

Upinzani wakataa matokeo, waitaka IEBC imtangaze Raila mshindi



https://ichef.bbci.co.uk/live-experience/cps/624/cpsprodpb/vivo/live/images/2017/8/10/23f7f8b0-cec8-4a0e-b2f2-15ef6de3dff9.jpg

NAIROBI- MUUNGANO wa upinzani nchini (NASA), umeendelea kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais yanayotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kwenye mtandao wake.
Viongozi wa muungano wa NASA, wamesema walikutana na wakuu wa Tume ya Uchaguzi Kenya na kuwasilisha rasmi malalamiko yao kupitia barua.
Ajenti Mkuu wa upinzani, Musalia Mudavadi, ambaye ni Naibu Waziri Mkuu wa zamani, amesema upinzani umepata maelezo zaidi kwamba matokeo ya uchaguzi yalivurugwa baada ya kudukuliwa kwa mitambo ya IEBC.
Wakuu wa IEBC wamekanusha kwamba mitambo ilidukuliwa. Mwenyekiti wa tume hiyo, Wafula Chebukati amesema kulikuwa na jaribio la kudukua mitambo hiyo, lakini halikufanikiwa.
Mudavadi amedai mgombea wao Raila Odinga ndiye aliyeshinda uchaguzi huo.
“Tunamtaka Mwenyekiti wa IEBC atangaze matokeo na kumtangaza Odinga na Kalonzo kama rais mteule na naibu rais mteule wa Kenya mara moja,” alisema Mudavadi huku akiwasisitiza Wakenya waendelee kuwa watulivu.
Kwa mujibu wa sheria nchini, ni kinyume cha sheria kwa mtu yeyote kutangaza matokeo au kusambaza matokeo ambayo hayajatoka kwa tume ya taifa ya uchaguzi.
Ni tume hiyo ya uchaguzi pekee ndiyo inayoruhusiwa kutangaza matokeo.
BBC

No comments

Powered by Blogger.