Header Ads

Tetesi Asubuhi; Chelsea wamnyatia Perisic # Griezman aitaka Man Utd # Liverpool wamtaka Insigne



http://e2.365dm.com/17/05/16-9/20/skysports-ivan-perisic-inter-milan_3965020.jpg?20170528151157

LONDON- BAADA ya kukumbana na kipigo cha bao 3-2 wikiendi hii, Chelsea wamepanga kumnyakua winga wa Inter Milan, Ivan Perisic (28) ambaye ni windo la muda mrefu la Man United. Mirror.

http://wallpapercave.com/wp/wp1816519.png
Mshambuliaji mahiri wa Atletico Madrid, Antoine Griezman (26) amesema ataangalia uwezekano wa kujiunga na Man United, endapo timu yake itaamua kumuuza kipa wao, Jan Oblak kwenda PSG. Hatua hiyo imeelezwa kutomfurahisha Mfaransa huyo. Don Ballon.

https://www.thesportsman.com/media/images/admin/football/Sergi_Roberto.jpg
Manchester United wamesema watakuwa tayari kutoa pauni milioni 36.5 (sh bilioni 105.8), kama ada ya kumnunua kiungo wa Barcelona, Sergi Roberto (25) endapo mchezaji huyo atasisitiza kuondoka Nou Camp. Don Ballon.

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/03/nintchdbpict000296088650.jpg?strip=all&w=960
Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema timu hiyo inatakiwa kufanya usajili kabla ya dirisha la usajili kufungwa, ili kuimarisha kikosi chao. Pia, Klopp amesema anamtaka Lorenzo Insigne (26) wa Napoli, ili kuziba pengo la Philippe Coutinho anayekwenda Barcelona. Express.

https://www.thisisanfield.com/wp-content/uploads/PA-29108698-600x400.jpg
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Juventus, Beppe Marotta amesema timu hiyo inavutiwa na windo la Liverpool linalokipiga RB Leipzig, Naby Keita (22). La Gazzetta dello Sport.

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2017/03/01/13/3DACC8C100000578-0-image-a-80_1488374163987.jpg
Beki wa Chelsea, Cesar Azpilicueta (27) amesema kuwa timu hiyo inahitajika ifanye usajili haraka kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili ili kukiimarisha kikosi chao kinachoonekana kuwa kidogo. Evening Standard.

https://metrouk2.files.wordpress.com/2016/03/498267664.jpg?w=748&h=497&crop=1
Tottenham wamesema wana mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Lazio, Keita Balde (22), baada ya mchezaji huyo kuachwa nje ya kikosi kilichocheza jana dhidi ya Juventus kwenye kombe la Supercoppa Italiana. Mirror.

http://e0.365dm.com/16/12/16-9/20/skysports-virgil-van-dijk_3860836.jpg?20161229154347
Chelsea imesema iko tayari kutoa dau la pauni milioni 50 (sh bilioni 145), kwa ajili ya kumsajili beki wa Southampton anayewindwa na Liverpool, Virgil van Dijk (26). Daily Star. 

Image result for Bruno Amorim
Manchester United wameeleza kuwa wamekaribia kuelewana maslahi binafsi na mshambuliaji kinda wa Oliveirense ya Ureno, Bruno Amorim (19). Daily Mail.


Leicester City imesema itakataa dau la pauni milioni 31.8 (sh bilioni 92.2), ambazo zitatolewa na AS Roma ya Italia, kama dau la usajili la Riyad Mahrez (26). Leicester wanataka pauni milioni 50 (sh bilioni 145). Mirror.

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/03541/barry_3541780b.jpg
Kocha wa Everton, Ronald Koeman amesema hataweza kuvumilia kuona kiungo wa timu hiyo, Gareth Barry (36) akiondoka klabuni hapo kwenye dirisha hili la usajili. Liverpool Echo.

http://thesefootballtimes.co/wp-content/uploads/2015/11/o-gylfi-sigurdsson-facebook.jpg
Kocha wa Swansea, Paul Clement amekitaka chama cha soka Uingereza (FA), kiweke utaratibu wa kufungwa kwa dirisha la usajili kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu. Kwa sasa, Clement anapambana kumbakiza kiungo Gylfi Sigurdsson (27). Daily Mail.

http://i4.mirror.co.uk/incoming/article10875403.ece/ALTERNATES/s615/Arsenal-Training-Session.jpg
Newcastle United imeongeza juhudi za kumnasa kiungo wa Arsenal, Jack Wilshere (25), baada ya mchezaji huyo kuachwa kwenye kikosi kilichoanza dhidi ya Leicester City. Sun.

No comments

Powered by Blogger.