Header Ads

Scaramucci: Kuna watu wanataka kumng’oa madarakani Trump



https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/117ED/production/_97316617_themooch.jpg

NEW YORK- OFISA wa Mawasiliano ambaye alidumu kwa muda mfupi katika ikulu ya Marekani, Anthony Scaramucci amesema kuna watu ndani ya Serikali ambao wanataka kumng’oa madarakani Rais Donald Trump.
Akizungumza na televisheni ya ABC, alisema Trump analengwa kwa sababu hakuwamo kati ya viongozi wa siasa nchini humo. Alipoombwa ataje majina, Scaramucci alisema ameshawataja na rais anahitaji kuleta watu zaidi walio watiifu kwake.
Alipohudumu kwa siku kumi, Scaramucci alikosoa watu kadhaa pamoja na mkuu wa ofisi ya rais wa zamani, Reince Priebus.
BBC

No comments

Powered by Blogger.