Header Ads

Hazard na Bakayoko waanza mazoezi Chelsea



http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2017/08/15/13/4345D17000000578-4792304-image-a-10_1502800109455.jpg

LONDON- HABARI njema kwa mashabiki wote wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu England (EPL), ni kwamba mshambuliaji wao machachari, Eden Hazard amerudi mazoezini baada ya kuwa nje kwa miezi miwili.
Hazard alionekana mazoezini leo, huku akionekana mwenye furaha na kuashiria kuwa amepona tatizo la kifundo cha mguu (ankle) ambalo lilimpata akiwa katika majukumu ya kuiwakilisha timu yake ya taifa, Ubelgiji.
http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2017/08/15/13/4345D23200000578-4792304-image-a-12_1502800175780.jpg
Licha ya Hazard ambaye aliumia mwezi Juni mwaka huu kurudi mazoezini, mshambuliaji mwingine wa timu hiyo, Pedro Rodriguez ameendelea kuwa nje kutokana na tatizo la kifundo cha miguu.
Kwa upande mwingine, kiungo mpya wa timu hiyo, Tiemoue Bakayoko alionekana akifanya mazoezi mepesi ambayo yanamaanisha kuwa anaendelea kupona taratibu baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti.
http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2017/08/15/13/4345D18700000578-4792304-image-m-15_1502800266244.jpg
Bakayoko
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Chelsea walionekana kupwaya zaidi baada ya kukumbana na kipigo cha bao 3-2 kutoka kwa Burnley.
Daily Mail.

No comments

Powered by Blogger.