Header Ads

Coutinho aomba kuondoka Liverpool



https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/03/nintchdbpict000310067442.jpg?strip=all&w=960&quality=100

LIVERPOOL- KWA mujibu wa mtandao wa shirika la habari la Sky Sports, mchezaji mahiri wa Liverpool, Philippe Coutinho (25) amewasilisha rasmi hati ya kuomba kuondoka klabuni hapo.
Sky Sports imeeleza kuwa habari hizo wamepewa na mmoja wa watu wa familia ya Coutinho, ambaye alidai kwamba; “Coutinho amejaribu kwa kadri awezavyo kutafuta kuondoka kwa njia njema, na ya urafiki lakini ameshindwa kabisa.”
“Anaipenda sana Liverpool na mashabiki wake, lakini kama ilivyokuwa kwa Steven Gerrard na Luis Suarez hawakuweza kuondoka kirafiki. Liverpool huwa hairuhusu wachezaji wake kuondoka kwa njia ya kirafiki.”
Kwa upande mwingine, Stock City imekamilisha usajili wa beki wa Uholanzi na Porto, Bruno Martins Indi kwa ada yenye thamani ya pauni milioni 7 (sh bilioni 20.3). Sky Sports.

No comments

Powered by Blogger.