Header Ads

Watu 40 wauawa uvamizi wa Boko Haram



Nigerian military vehicle

MAIDUGURI- WATU 40 wameuawa, katika jaribio la kuwaokoa mateka wa kundi la wanamgambo la Kiislamu la Boko Haram.
Takriban watu watano wa kampuni ya kuchimba mafuta waliuawa, kwa mujibu wa chuo cha Maiduguri.
Wanajeshi pia waliuawa wakati wa uvamizi huo. Idadi hiyo kubwa ya vifo, ni pigo kwa Serikali ambayo inasisitiza kuwa kundi la Boko Haram limeshindwa.
Taarifa za kina kuhusu kile kilichotokea Jumanne hazijulikani, huku ripoti za awali kutoka kwa jeshi, zikisema kuwa watu ambao walitekwa ni pamoja na wafanyakazi wa chuo cha Maiduguri ambao hata hivyo waliachiwa.
Jeshi lilisema kuwa miili ya wanajeshi 9 na raia mmoja, ilipatikana katika eneo la tukio Jumanne.
Lakini sasa chuo hicho kimesema kuwa, takriban wafanyakazi watano wakiwemo wasomi wawili na dereva waliuawa wakati msafara wao uliokuwa chini ya ulinzi mkali, uliokuwa ukirejea ulipovamiwa huku.
Takriban watu 20,000 wameuawa na maelfu ya wengine kutekwa tangu Boko Haram ianzishe harakati zake mwaka 2009.
Katika kisa kibaya zaidi Boko Haram, waliteka wasichana 276 kutoka shule ya wasichana ya Chibok iliyopo Kaskazini Mashariki mwa nchi mwaka 2014. Tangu wakati huo, wamewaachilia zaidi ya wasichana 100 kubadilishana na wapiganaji.
BBC

No comments

Powered by Blogger.