Ukosefu wa bangi wasababisha hali ya tahadhari kutangazwa Nevada

NEVADA-
MAOFISA wa Serikali jimboni hapa, wametangaza kuanza kuchukua hatua za dharura za
kukabiliana na uhaba wa bangi.
Hali hiyo
inatokana na mahitaji kuwa ya juu, tangu bangi ihalalishwe kwa matumizi ya
kujiburudisha mwanzoni mwa mwezi huu. Uhaba huo unadaiwa kuchangiwa kwa kiasi
kikubwa na uchache wa wauzaji wa mmea huo.
Sheria
iliwapa wauzaji wa pombe ruhusa ya kuuza bangi, lakini wengi hawatimizi mahitaji
ya leseni kuweza kuuza bidhaa hizo.
Idara ya
kodi jimboni hapa, ilitangaza dharura inayomaanisha kuwa maofisa watachukua
hatua za dharura kukabiliana na uhaba huo.
Mauzo ya
karibu dola milioni 3 (sh bilioni 6.6), yalikadiriwa siku nne za kwanza baada
ya matumizi ya bangi kuhalalishwa. Nevada ilipiga kura ya kuhalalisha matumizi
ya bangi kwa burudani Novemba mwaka jana, kufuatia hatua kama hizo katika
majimbo mengine.
Matumzi ya
bangi kwa matibabu yameruhusiwa katika majimbo 25 ikiwemo Nevada, ambapo
imehalalishwa tangu nwaka 2001.
BBC
No comments