Header Ads

Rushwa yamponza rais wa zamani Brazil



Brazil

BRASILIA- RAIS zamani wa Brazil, Luiz Ignacio Lula da Silva (pichani), amehukumiwa kifungo cha miaka tisa na miezi sita jela kutokana na kesi tano za ulaji rushwa zinazomkabili.
Kiongozi huyo wa zamani wa chama cha muungano, alijizolea umaarufu kutoka jamii ya kimataifa kwa sera zake za kijamii ambazo zilisaidia kuboresha maisha Brazil.
Lakini sasa, mambo yamegeuka na kukutwa na hatia ya kukubali hongo ya zaidi ya dola milioni 1 za malipo ya ghorofa la mapumziko kwa ajili ya ukarabati wake kwa kampuni ya ujenzi ya Kibrazil, iitwayo kwa kifupi OAS.
Hukumu hii inakuja wakati ambapo, Lula ametoa msimamo mkali kwamba ana mpango wa kuingia katika kinyang'anyiro cha kugombea nafasi ya urais mwakani.
Kufuatia hukumu hiyo, rais huyo amekana mashtaka yote yanayomkabili kwa kudai kuwa hajafanya makosa yoyote kiasi cha kustahili hukumu hiyo, huku mawakili wanaomtetea wakiapa kukata rufaa.
Wakati huo huo, kamati ya Bunge la Congress ya Brazil, inajadili iwapo iiruhusu Mahakama Kuu kusikiliza kesi ya rushwa inayomhusisha Rais Michel Temer.
Temer alishtakiwa mwezi uliopita, kwa tuhuma za kupokea hongo kutoka kampuni kubwa ya usindikaji nyama.
Kamati hiyo inatarajiwa kupiga kura hapo kesho. Iwapo pendekezo hilo litapita, suala hilo litajadiliwa katika bunge dogo la wawakilishi, ambapo theluthi mbili itahitajika kupiga kura ili Rais ashitakiwe.
BBC

No comments

Powered by Blogger.