Ujumbe wa mtandaoni wavunja ndoa Taiwan

TAIPEI- Umewahi kupuuza ujumbe wa mpenzi au mchumba wake
kwenye mitandao ya kijamii? Basi unapaswa uelewe kwamba ujumbe huo unaweza
ukatumika kama ushahidi ambao utasababisha uhusiano au ndoa yenu ivunjwe na
mahakama.
Mwanamke
mmoja nchini, ameruhusiwa kumpa talaka mume wake, kwa kutumia ishara kwamba
ujumbe wake aliomtumia mumewe ulisomwa kama ushahidi kwamba mumewe alimpuuza.
Mtandao wa
kijamii wa Line unaonesha mumewe alikuwa akifungua ujumbe huo, lakini hakujibu.
Ushahidi huo, umesababisha Jaji ambaye alikuwa akisikiliza shauri hilo amkubalie
mwanamke huyo ombi la kumtaliki mumewe.
Mwanamke huyo
alitumia alama za rangi ya bluu, ambazo hutumiwa na mitandao kama vile Line na
WhatsApp mtu anaposoma ujumbe, kudai kwamba mumewe alikuwa ameupokea ujumbe.
Jaji Kao wa mahakama
ya masuala ya kifamilia, Hsinchu, amesema hali kwamba mwanamume huyo alipuuza
ujumbe huo, ni ushahidi kwamba ndoa kati ya wawili hao haiwezi ‘kuokolewa’ na
vyombo na kuwaruhusu kupeana talaka.

Katika
kipindi cha miezi sita hivi, mwanamke huyo ambaye jina lake la ukoo ni Lin,
alimtumia mumewe ujumbe mara kadhaa, wakati mmoja ikiwa ni baada ya kulazwa
hospitalini baada ya kupata ajali barabarani.
Katika
ujumbe mmoja, alimwambia mumewe kwamba alikuwa katika chumba cha dharura
hospitalini na akamuuliza ni kwa nini anasoma ujumbe wake lakini hamjibu.
Ingawa
mumewe alimtembelea hospitalini mara moja, mahakama ilisema kwamba kitendo cha
kupuuza ujumbe huo ni msingi tosha wa kumpa talaka.
“Mshtakiwa
hakumjulia hali mlalamishi, na habari aliyotumiwa na mlalamishi aliisoma lakini
hakujibu,” mahakama ilisema kwenye uamuzi wake.
Ilikuwa ni
baada ya mwezi mmoja au miwili hivi, baada ya ajali hiyo, ndipo mumewe
alimtumia ujumbe mfupi.
“Ujumbe wake
ulikuwa unamhusu mbwa wao, na alimfahamisha pia kwamba kulikuwa na barua
iliyotumwa kwake, lakini hakuonesha ishara za kutaka kujua hali yake,” Jaji Kao
alisema.
Wawili hao
walifunga ndoa 2012. Mwanamke huyo ambaye amewahi kuolewa awali ana miaka 50
hivi na mumewe ana miaka 40 hivi.
BBC
No comments