Header Ads

Tetesi za usajili; Man Utd kutoa £166m kwa Lukaku na Morata # PSG yatoa £ kwa Coutinho # Atletico Madrid yaweka £ 22m kwa Costa



https://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2017/02/10/15/romelu-lukaku.jpg

LONDON- KLABU ya Manchester United wanakaribia kufanya uhamisho wao mkubwa wa majira ya kiangazi, kutokana na timu hiyo kujiandaa kuipiku Chelsea kwa kumsajili Romelu Lukaku kutoka Everton kwa dau la pauni milioni 100 (sh bilioni 290). Daily Mail
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/03/nintchdbpict0003072985002-e1490376791948.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Gazeti la Marca la Hispania, linaripoti kuwa Man United wameweka mezani kwa Real Madrid dau la pauni milioni 66 (sh bilioni 191.4) kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji Alvaro Morata (24).
http://i1.mirror.co.uk/incoming/article10478096.ece/ALTERNATES/s615/Liverpool-v-Middlesbrough-Premier-League.jpg
PSG ya Ufaransa, wametangaza kuwa tayari kutoa dau la pauni milioni 70 (sh bilioni 203), kwa ajili ya kupata huduma ya kiungo wa Liverpool ya Uingereza, Philippe Coutinho (25) ambaye msimu uliopita alitikisa nyavu mara 13. Daily Express.
https://images.cdn.fourfourtwo.com/sites/fourfourtwo.com/files/styles/image_landscape/public/costa-main_0.jpg?itok=cc83RXW6&c=b5573862cced0966947d6647769b4219
Atletico Madrid wanajiandaa kutoa dau la pauni milioni 22 (sh bilioni 63.8) ili kuipata tena huduma ya Diego Costa (28) ambaye anatarajiwa kuuzwa Chelsea muda wowote. Guardian.
https://www.arsenal.com/sites/default/files/styles/large_16x9/public/images/laca2.jpg?itok=-7i0huWO
Kocha wa zamani wa Liverpool, Gerard Houllier, amesema anaamini Arsenal wanaweza wakawa wamempata ‘Ian Wright’ mpya baada ya kumnasa mshambuliaji, Alexandre Lacazzette (26) kutoka Olympic Lyon. TalkSport.
http://www.thegunners247.uk/resources/as7980.jpg?timestamp=1439822344007 
Mshambuliaji wa Arsenal, Alexis Sanchez (28) amesema anataka mshahara wa pauni 400,000 (sh bilioni 1.16) ili aweze kubakia klabuni hapo, ikiwa ni ongezeko la pauni 125,000 (sh milioni 262.5) kutoka mshahara wake wa sasa. Daily Miror.
http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2016/0227/r58461_1296x729_16-9.jpg&w=738&site=espnfc
West Ham United wanaongoza mbio za kumsajili mshambuliaji wa Burnley, Andre Gray (26) kwa dau la pauni milioni 15 (sh bilioni 43.5). mchezaji huyo amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake. Evening Standard.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/07/nintchdbpict000336448201.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Wageni wa Ligi Kuu, Huddersfield wako karibu kabisa kukamilisha usajili wa mlinzi wa kati wa FC Copenhagen, Mathias Jorgensen kwa dau la pauni milioni 3.5 (sh bilioni 10). The Sun.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/07/nintchdbpict000334835911.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Kiungo wa Chelsea, Nathaniel Chalobah (22) anafanya mazungumzo na klabu ya Watford kwa ajili ya kujiunga nayo kwa ada ya pauni milioni 5 (sh bilioni 14.5). Daily Miror.

Asante kwa kuwa nasi na kwa heri hadi hapo jioni tena 

No comments

Powered by Blogger.