Tesla yaanza kuuza magari ya umeme kwa wafanyakazi wake
![https://media4.s-nbcnews.com/j/newscms/2017_30/2088441/2017-07-13t011046z_1946549674_rc1be3758c10_rtrmadp_3_usa-funds-tesla_99f4c60bd337d6b6eccc3ce04b02a7ae.nbcnews-ux-600-480.jpg](https://media4.s-nbcnews.com/j/newscms/2017_30/2088441/2017-07-13t011046z_1946549674_rc1be3758c10_rtrmadp_3_usa-funds-tesla_99f4c60bd337d6b6eccc3ce04b02a7ae.nbcnews-ux-600-480.jpg)
CALIFORNIA-
MKURUGENZI wa kampuni ya Tesla, Elon Musk amesema ilikuwa ni vigumu kwao
kutengeneza aina ya magari ya kutumia umeme ambayo yamekamilika kwa sasa.
Kauli
hiyo ya Musk imekuja katika wakati ambapo baadhi ya mataifa kama Ufaransa na
Uingereza, tayari yameeleza kuwa mwisho wa magari yanayotumia mafuta ni 2040.
Tayari
Tesla imekamilisha magari 30, ambayo yalitolewa jana ili kuanza kuuzwa kwa
wanunuzi ambao ni wafanyakazi wa kampuni hiyo.
Nje
ya ya jengo la Tesla katika eneo la Fremont, Musk alionesha magari hayo ambayo
yatauzwa kwa dola 35,000 (sh milioni 77) yenye uwezo wa kukimbia umbali wa
kilometa 350 kwa saa.
Kabla
ya tukio hilo, Musk alikiri kuwa ilikuwa vigumu zaidi na iliwachukua muda na
rasilimali kuweza kukamilisha utengenezaji wa magari hayo yaitwayo Model 3.
“Kwa
kweli ilikuwa ni changamoto kubwa. Tunatarajia kupita katika kipindi kingine
cha miezi sita migumu, ambayo ni sawa na kutengeneza kuzimu ili kukamilisha utengenezaji
wa magari mengine,” alisema Musk.
NBC
News
No comments