Header Ads

Marekani yadai itatumia nguvu za kijeshi dhidi ya Korea Kaskazini iwapo italazimika



Balozi wa Marekani katika Umoja wa mataifa Nick Haley
WASHINGTON DC- MAREKANI imesema kuwa itatumia nguvu za kijeshi dhidi ya Korea Kaskazini, ‘iwapo ni lazima’ kufuatia jaribio la kombora la masafa marefu lilotekelezwa na taifa hilo.

Balozi wa Marekani, Nikki Haley (pichani) alisema kuwa maamuzi mapya pia yatawasilishwa dhidi ya Korea Kaskazini katika Umoja wa Mataifa (UN).
Alielezea jaribio hilo kama tishio la kijeshi mbali na kutishia kutumia vikwazo vya kibiashara. Jaribio hilo la kombora la hivi karibuni, ni miongoni mwa majaribio mengine yanayokiuka marufuku ya UN.
Wakati huohuo, Waziri wa Ulinzi nchin,i James Mattis na mwenzake wa Japan, Tomomi Inada, walisema kuwa jaribio hilo ni uchokozi ambao hautakubalika.
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ulinzi imesema kuwa, wawili hao walizungumza kwa njia ya simu ambapo Jenerali Mattis alisema Marekani itaendelea kuilinda Japan.
Haley alisema jana kwamba, jaribio la kombora la masafa marefu la Korea Kaskazini (ICBM) linaangamiza suluhu ya uwezekano wa mazungumzo ya kidiplomasia
“Marekani imejiandaa kutumia uwezo wake wote kujilinda na washirika wetu,” Haley aliliambia baraza la usalama katika Umoja wa Mataifa, ambalo lilikutana kwa kikao cha dharura kuzungumzia hatua hiyo ya Korea Kaskazini.
“Moja ya uwezo wetu upo katika jeshi. Tutautumia iwapo tutalazimika kufanya hivyo, lakini tungependelea kutoelekea upande huo,” alisema.
Haley ambaye alieleza kuwa alijadiliana na Rais Donald Trump, alisema kuwa Marekani pia inaweza kukata biashara na mataifa ambayo yanaendelea kufanya biashara na Korea Kaskazini kwa kukiuka maamuzi ya UN.
“Tutayaangazia mataifa ambayo yanaendelea kufanya bishara na utawala huu usiofuata sheria,” alisema.
BBC

No comments

Powered by Blogger.