Header Ads

Marekani na Urusi zajadiliana kuhusu majengo



Majengo ya Urusi yanayoshikiliwa na Marekani
Majengo ya Urusi yanayoshikiliwa na Marekani.

WASHINGTON DC- Mazungumzo kati ya maofisa waandamizi wa Marekani na Urusi kuhusu madai ya Urusi kutaka kurudishiwa majengo yake yamemalizika mjini hapa.
Katika madai hayo, Urusi inadai kurudishiwa majengo yake mawili ya Kibalozi ambayo yalitwaliwa na utawala wa Rais mstaafu, Barrack Obama, mnamo Desemba mwaka jana kutokana na kudaiwa kutumika kuipeleleza Marekani.
Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kwa Waandishi wa Habari, lakini walipoulizwa na Wanahabari waliokuwa wakisubiri kujua hatma ya mazungumzo yao, maofisa wa Urusi walijibu kwa kifupi kwa kusema “takriban yote yamefikiwa.”
Awali, Urusi ilionya kuchukua hatua ya kulipiza kisasi iwapo vifaa katika majengo hayo vinawekwa tena. Maeneo na majengo hayo, yalikuwa yakishikiliwa na Marekani kutokana na madai kuwa yalikuwa yakitumiwa kwa shughuli za kiitelejensia
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov ameishutumu Marekani kwa kile alichokiita ‘Wizi wa wazi.’
Hali ya kisiasa nchini, imekuwa mbaya katika wakati pia uchunguzi juu ya Urusi kuingilia kati uchaguzi wa Rais ukiendelea.
BBC

No comments

Powered by Blogger.