Mafuriko yaua watu 8 China

NANNING— WATU
nane wamekufa na wengine zaidi ya 250,000 kupoteza mali zao, baada ya nyumba
zao kukumbwa na mafuriko makubwa ambayo yamesababishwa na mvua zinazoendelea
kunyesha Kusini mwa nchi.
Kwa mujibu
wa taarifa iliyotolewa na mamlaka za mji wa Guangxi Zhuang, watu tisa
wanaripotiwa kupotea huku wengine 34 kujeruhiwa baada ya mafuriko kuvunja zaidi
ya nyumba 600 na kuharibu hekta 17,000 za mazao.
Hata hivyo,
tayari wananchi zaidi ya 38,000 wamefanikiwa kuhamishwa na kupelekwa katika
maeneo salama yenye huduma mbalimbali za kijamii kama vile malazi, huduma za
afya, maji na chakula.
Mwishoni mwa
wiki, Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa nchini (NMC), ilieleza kuwa mvua kubwa
zinatarajiwa kunyesha Jumapili na Jumatatu usiku katika miji ya Guangxi na
Hunan.
Xinhua
No comments