Korea Kaskazini: Kombora letu la Hwasong 14 linafika Marekani
![North Korean leader Kim Jong-un reacts during test launch in undated photo released by North Korea's Korean Central News Agency on May 15, 2017](https://ichef.bbci.co.uk/news/660/cpsprodpb/184AE/production/_97120599_040837567.jpg)
PYONGYANG- SERIKALI imesema jaribio la kombora la masafa
marefu, lililofanyika jana limeonesha mafanikio makubwa na pia limedhihirisha
lina uwezo wa kufika Marekani.
Aidha,
Serikali imeeleza kuwa mafanikio ya kombora hilo la Hwasong 14 lenye uwezo wa
kuruka kutoka bara moja hadi jingine (ICBM), ni onyo kwa taifa hilo la Amerika
Kaskazini.
![https://ichef-1.bbci.co.uk/news/624/cpsprodpb/169BA/production/_97120629_mediaitem97116954.jpg](https://ichef-1.bbci.co.uk/news/624/cpsprodpb/169BA/production/_97120629_mediaitem97116954.jpg)
Kombora la Hwasong 14
Akizungumza mara
baada ya tukio hilo, Rais Kim Jong-un alisema jaribio hilo la Hwasong 14 limethibitisha
kuwa linaweza kupiga sehemu yoyote ya Marekani.
Ni wiki tatu
ndizo zilizopita tangu kufanyika kwa jaribio la kombora lingine, lakini hili
limeonesha mafanikio zaidi ya lile la Julai 3, mwaka huu ambalo nalo
liliangukia sehemu ya bahari karibu na Japan.
Akithibitisha
jaribio hilo, Rais Kim Jong-un alisema kombora hilo lilisafiri umbali wa
kilometa 3,724 juu angani kwa muda wa dakika 47 pekee.
Katika
kujibu mapigo, Korea Kusini na Marekani nazo zilifanya majaribio ya makombora
maalum ambayo yalidondokea kwenye maji yaliyo kwenye umiliki wa taifa hilo la
jirani.
Waziri wa
Ulinzi wa Korea Kusini,Song Young-moo alisema wanaandaa njia huru za kudhibiti vitisho
vya Korea Kaskazini na wataharakisha usimikaji wa mitambo ya kutungua makombora
kutoka Marekani iitwayo THAAD.
BBC.
No comments