Kombora la Korea Kaskazini linaweza kufika Marekani

WASHINGTON
DC- MAREKANI imethibitisha kwamba Korea Kaskazini ilifanya jaribio la kombora
la masafa marefu (Hwasong -14), ambalo kulingana na wataalama wanaamini linaweza kufika katika
jimbo la Alaska nchini.
Waziri wa Mambo
ya Nje nchini, Rex Tillerson amelitaja jaribio hilo kuwa vitisho vipya kwa
Marekani na dunia na kuonya kwamba Serikali haitakubali hatua ya Korea
Kaskazini kujihami na nyuklia.
Korea
Kaskazini imedai jana kwamba, ilifanikiwa kulifanyia majaribio kombora lake la
masafa marefu ICBM. Wakijibu, Marekani na Korea Kusini zilirusha makombora Kusini
mwa maji Korea.
Zoezi hilo
la kijeshi la pamoja lililenga kuonesha uwezo wa mashambulizi ya mataifa hayo
mawili, Pentagon ilisema. Ijapokuwa jaribio la jana lilionekana kuwa hatua
kubwa, wataalam wanaamini kwamba Korea Kaskazini haina kombora la masafa marefu
la kinyuklia.
Tillerson,
pia alionya kwamba taifa lolote ambalo linasaidia kiuchumi na kijeshi Korea Kaskazini
ama limefeli kuidhinisha kwa ukamilifu maamuzi ya Baraza la Usalama ya Umoja wa
Mataifa, linasaidia utawala hatari.
Marekani
imetaka kufanyika kwa mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa
Mataifa kujadili suala hilo. Mkutano wa faragha wa wanachama wa baraza hilo,
unatarajiwa baadaye leo.
Je Korea
kaskazini ilisema nini jana?
Tangazo katika
runinga ya taifa ya Korea Kaskazini lilisema kuwa, kombora hilo aina ya Hwasong
-14 linaloweza kurushwa kutoka bara moja hadi jingine lilisimamiwa na kiongozi
wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un.
Ilisema kuwa
kombora hilo liliruka umbali wa kilomita 2,802, na kusafiri kwa umbali wa
kilomita 933 kwa dakika 39 kabla ya kuanguka baharini.
Korea
Kaskazini imesema kuwa ni taifa lililojihami kinyuklia, ambalo linamiliki
kombora la masafa marefu linaloweza kushambulia eneo lolote duniani.
Shirika la Habari
cha Korea Kaskazini (KCNA), baadaye lilimnukuu Rais Kim Jong-un akisema kuwa
jaribio hilo ni zawadi kwa Wamerakani siku yao ya uhuru. Jaribio hilo ambalo ni
miongoni mwa majaribio ya makombora yake, linakiuka marufuku ya baraza la
usalama la Umoja wa Mataifa.
Lakini
wataalam wengi wanaamini kwamba, Korea Kaskazini bado haijakuwa na uwezo wa
kutengeza kichwa cha kinyuklia kinachoweza kutosha katika kombora la masafa
marefu na kwamba kombora kama hilo haliwezi kushambulia eneo linalolenga.
Je kombora
hilo lina uwezo wa kusafiri umbali gani?
Swali kuu ni
linaweza kusafiri kwa umbali gani, alisema mwandishi wa BBC Evans Seoul.
Je linaweza
kushambulia Marekani?
David Wright,
kutoka muungano wa kisayansi anasema kuwa iwapo ripoti hiyo ni ya sawa, kombora
hilo linaweza kusafiri kwa umbali wa kilomita 6,700.
“Umbali huo
unaweza kulifanya kufika Alaska, lakini sio visiwa vya Hawaii ama hata majimbo
mengine 48 ya Marekani. Siyo kombora la pekee ambalo Korea Kaskazini itahitaji,”
alisema.
Pia aliongeza
kuwa, ni lazime taifa hilo liwe na uwezo wa kulinda kichwa cha nyuklia
kinapopaa angani na sio wazi iwapo lina uwezo huo.
BBC
No comments