Header Ads

Mourinho ataka kukaa Man United miaka 15



https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2016/07/nintchdbpict000252557418-e1468918117127.jpg?w=960&strip=all

LOS ANGELES- KOCHA Jose Mourinho anataka kufuata nyayo za Sir Alex Ferguson katika timu ya Manchester United kwa kuinoa kwa miaka mingi.
Akizungumza katika kambi ya maandalizi ya timu yake kwa msimu mpya kwenye Uwanja wa UCLA nchini Marekani, Mourinho alisema juzi anataka kuinoa timu hiyo yenye maskani yake Old Trafford kwa miaka 15.
Mourinho (54) anainoa United kwa msimu wa pili huku akiwa hajafanya mabadiliko katika benchi lake la ufundi amesema anataka kuinoa United kwa miaka mingi kama Ferguson kisha kustaafu.
“Niko tayari kwa hili. Ningependa kusema niko tayari kwa miaka 15. Hapa? Ndiyo kwa nini isiwe hivyo? Ninakiri inaweza kuwa ngumu sana kwa sababu ya presha inayozunguka kazi yetu,”
“Kila mtu amekuwa akiweka presha kwa makocha na watu wakisema tunatakiwa kushinda, lakini kwa kweli mmoja kuweza kushinda kila mwaka inakuwa ngumu sana,'' alisema.

No comments

Powered by Blogger.