Header Ads

Jioni Njema; No ofa kwa Aubameyang # Chelsea yamgeukia Danilo # Prince wa Monaco asema Mbappe haondoki # Dier hauzwi



https://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2016/12/07/17/pierre-emerick-aubameyang.jpg

BERLIN- BORUSSIA Dortmund imesema hakuna ofa yoyote iliyowasilishwa mezani mwa klabu hiyo, ikiwa ni sehemu ya usajili wa mshambuliaji wao, Pierre-Emerick Aubameyang.
Kauli hiyo inakinzana na ile ya Chelsea ambao wamedai kutoa pauni milioni 70 (sh bilioni 203) ili kumpata mchezaji huyo. Pia, inadaiwa kuwa wakala wake amefanya mazungumzo na PSG ya Ufaransa na AC Milan ya Italia.
http://as00.epimg.net/futbol/imagenes/2017/01/19/copa_del_rey/1484818902_514198_1484819006_noticia_normal.jpg
Chelsea imedaiwa kufanya mazungumzo na Real Madrid, kwa ajili ya kumsajili mlinzi wao wa kulia, Danilo, ambaye anatakiwa na Juventus pia.
Sky Sports imeelezwa kuwa, itawalazimu Chelsea kutoa pauni milioni 30 (sh bilioni 87) kwa ajili ya kuipata huduma ya beki huyo.
http://s.newsweek.com/sites/www.newsweek.com/files/styles/embed-lg/public/2017/04/25/kylian-mbappe.jpg
Mwanamfalme Prince II wa Monaco, anaamini kuwa staa wa timu ya Monaco, Kylian Mbappe atabakia klabuni hapo na kusaini mkataba mpya.
Alipoulizwa kama Mbappe anaweza akaondoka msimu huu, mwanamfalme huyo alisema; “Sidhani kama hilo litatokea. Kuna mazungumzo yanaendelea na yananipa uhakika kuwa atabaki.”

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/04/nintchdbpict000318684421.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Sky Sports imeelezwa kwamba, Eric Dier hauzwi nab ado Tottenhma Hotspurs haijapokea ofa yoyote inayomhusu kiungo huyo. Licha ya kuwepo kwa madai kuwa Man United inamhitaji kwa udi na uvumba, vyanzo hivyo vinadai kuwa klabu hiyo inapoteza muda wake.
http://e2.365dm.com/17/05/16-9/20/skysports-ivan-perisic-inter-milan_3965020.jpg?20170528151157
Man United imeongeza nguvu kwenye dili la uhamisho la winga wa Inter Milan ya Italia, Ivan Perisic, ili kukamilisha usajili huo kabla ya wiki ijayo lakini Inter wamekaza kuwa bei yake ni pauni milioni 48 (sh bilioni 139.2).
http://ste.india.com/sites/default/files/2015/03/13/334614-victor-vitolo-cel-700.jpg
Atletico Madrid wametangaza kukamilisha dili la kumsajili mshambuliaji wa Sevilla, Vitolo kwa mkataba wa miaka 5. Hata hivyo, mchezaji huyo ataenda kucheza kwa mkopo Las Palmas hadi Januari mwakani kutokana na timu hiyo kuzuiwa na FIFA.
https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2017/07/nintchdbpict000328850866.jpg?strip=all&w=960&quality=100
Klabu ya PSG inatarajiwa kumtangaza muda wowote Dani Alves kuwa mchezaji wao, baada ya kukamilisha usajili wake mapema leo na tayari ameshatua Paris.



No comments

Powered by Blogger.