Header Ads

Jeshi la Kenya lawasaka Al Shabaab msitu wa Boni Kenya



Image result for KDF in Boni Forest
LAMU- JESHI la Ulinzi Kenya (KDF), limetuma vikosi kadhaa vya wanajeshi wake, katika msiu wa Boni mjini hapa ili kuwasaka wanamgambo wa Al Shabaab ambao jana walijaribu kuteka kituo cha polisi cha Pandaguo.

Hata hivyo, inatarajiwa kuwa KDF itapata wakati mgumu kutekeleza zoezi lao wa kuwasaka na kuwabaini wanamgambo hao, kwani wenyeji wa eneo hilo wamekuwa kimya bila kuoa taarifa zozote licha ya wapiganaji hao kudaiwa kuswali katika moja ya misikiti ya hapo kabla ya kushambulia kituo. 
Inadaiwa kuwa, wanamgambo hao walifika msikitini hapo majira ya saa 11 asubuhi na kuswali swala ya asubuhi msikitini hapo kabla ya kuanza kuelekea kwenye utekelezaji wa unyang’anyi wao. 
Baada ya kutoka msikitini hapo, wanamgambo hao walielekea kituo cha polisi cha Pandaguo na wengine kwenye zahanati iliyo karibu na kupora dawa na silaha kisha kutokomea. 
Wanakijiji wameeleza kuwa walisikia milipuko kadhaa nyakati za asubuhi leo, wakati KDF wakiendelea kutekeleza zoezi lao la kuwasaka wanamgambo hao ambao wanadaiwa kufikia 150 walivamia kituo na kukimbilia msituni humo.

Standard Newspaper

No comments

Powered by Blogger.