Header Ads

China; Manowari ya Marekani kukaribia kisiwa cha Triton ni uchokozi mkubwa



The USS Stetham, in a photo from 2015, arrives at a port in Shanghai 
Manowari ya USS Stethem
BEIJING- CHINA imetaja hatua ya manowari ya Marekani kupita karibu na kisiwa kinachozozaniwa Kusini mwa bahari ya China, kuwa uchokozi mbaya wa kisiasa na kijeshi.

Manowari ya USS Stethem ilipita karibu na kisiwa kinachozozaniwa cha Triton, ambacho ni moja ya visiwa vinavyodaiwa na China na nchi zingine.
Mara baada ya manowari hiyo ya Marekani kupita hapo, China ilijibu hatua hiyo haraka kwa kutuma melivita na ndege kwenda kisiwani humo.
Kisa hicho kilitokea muda mfupi, kabla ya viongozi wa nchi hizo mbili kufafanya. Marekani mara kwa amara imeionya China dhidi ya hatua yake ya kunyakua visiwa katika maeneo yanayozozaniwea, lakini China inasema inafanya hivyo kuambatana na haki zake.
China inasema kuwa itafanya kila iwezalo kulinda usalama wake. Pia imeilaumu Marekani kwa kuchochea vurugu eneo hilo, kwa kuwa uhusiano kati ya China na majirani wake wa Kusini mwa bahari ya China umeimarika.
Kisiwa hicho kidogo pia kinadaiwa na Vietnam na Taiwan. China imekuwa kwenye mzozo wa umiliki wa maeneo ya bahari na majirani zake kadhaa miaka ya hivi karibuni.


No comments

Powered by Blogger.