Header Ads

Ajali ya ndege yaua watu 16 Marekani



A still image showing a crashed plane in flames in a field, taken from video footage
MISSISSIPI- TAKRIBAN watu 16 wamefariki duniakwenye ajali ya ndege ya jeshi, ambayo imetokea jimboni hapa.

Ajali hiyo ilitokea katika kaunti ya LeFlore karibu kilometa 160 kusini mwa mji mkuu wa jimbo hilo, Jackson. Watu wote 16 waliokuwa ndani ya ndege hiyo waliangamia.
Hakuna taarifa rasmi zilizotolewa kuhusu kilichosababisha kutokea ajali hiyo. Kwa mujibu wa jarida la jimbo la Mississipi, ndege hiyo ilianguka katika shamba moja na mabaki yake yakatapakaa eneo lote.

No comments

Powered by Blogger.