Header Ads

Simba waendelea kutoroka mbugani Afrika Kusini



A lion in Kruger National Park, South Africa. 22 July 2010
MPUMALANGA- WALINZI wa mbuga ya Kruger, wanawattafuta simba wanne wa kiume ambao wametoroka kwenye mbuga hiyo.

Simba hao walitoroka mbugani hapo Jumapili, na mara ya mwisho walidaiwa kuonekana katika kijiji cha Matsulu. Usimamizi wa mbuga hiyo sasa umewataka wenyeji kuchukua tahadhari
Bado haijabainika ni kwa namna gani wanyama hao, walifanikiwa kutoroka na kutoka nje ya mbuga hiyo inayozungukwa na uzio mkubwa.
Mbuga ya kitaifa ya Kruger ni moja ya mbuga kubwa zaidi barani Afrika ikiwa na ukubwa wa kilomita 19.485 mraba.
Kisa hiki kinatokea baada ya simba wengine watano kutoroka mbuga hiyo Mei, mwaka huu. Wanne walipatikana lakini mmoja bado hajulikani aliko.
BBC

No comments

Powered by Blogger.