Header Ads

Picha mbalimbali za maandalizi ya Messi kufunga ndoa leo

Lionel Messi joined on the pitch by Antonella Roccuzzo and their two sons


Mshambuliaji wa timu ya Barcelona, Lionel Messi akiwa na mpenzi wake, Antonella Roccuzzo na watoto wao, Thiago (mkubwa) na Mateo (mdogo). Messi anatarajiwa kumuoa Antonella leo huko Rosario nchini Argentina.


Rosario's Hotel CityCenter set up for a previous event

Sehemu ya hoteli ya Rosario Hotel City Center ambako Lionel Messi anatarajiwa kufungia ndoa na mwenza wake, Antonella Roccuzzo, ambaye (Messi) alikutana naye akiwa na miaka mitano. Hoteli hiyo ipo katika mji wa Rosario ambao ndiko alikozaliwa staa huyo.
Uruguayan footballer Luis Suárez touches down in Rosario for teammate's big day  
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Uruguay na Barcelona, Luis Suarez akiwasili mjini Rosario kwa ajili ya kuhudhuria harusi ya rafiki yake mkubwa, Lionel Messi ambayo inatarajiwa kufanyika leo.
Mbali na Luis Suarez, staa mwingine ambaye aliambatana nao ni Neymar kutoka Brazil. Hata hivyo, inadaiwa kuwa nguli huyo wa Barca hakumwalika kocha wake wa zamani, Pep Guardiola na mfalme wa soka wa Argentina, Diego Maradona.
 

No comments

Powered by Blogger.