Header Ads

Mwanamke azirai baada ya kuvunja bangili ya milioni 96 China



the broken jade bracelet
YUNNAM- MWANAMKE mmoja nchini, amejikuta akizirai akiwa kwenye duka la kuuza vito vya thamani baada ya kuvunja kimakosa bangili ghali yenye thamani ya dola 44,000 (sh milioni 96.8).

Mtalii huyo kutoka mkoa wa Jiangxi, alikuwa akijaribu kuvaa bangili hiyo kwenye duka moja lililo mkoani hapa, karibu na mpaka na Myanmar. Alipoambiwa thamani na bangili hiyo, aliivua kwa haraka, lakini ikaanguka kimakosa na kuvunjika.
Hakuna makubaliano yaliyoafikiwa kuhusu namna ambayo bangili hiyo itafidiwa. Wafanyakazi wa duka walijaribu kumtuliza baada ya kisa hicho, lakini mara moja alianza kutokwa na jasho na kisha akazirai.
Alipata nafuu wakati wateja wangine ambao walikuja kumsaidia walipomfinya pua yake. Wafanyakazi wa duka walimwambia alipe dola 25,000 ili kutatua suala hilo, lakini yeye alidai kuwa alikuwa na dola 1,500 tu.
Polisi walishindwa kushawishi pande zote kufikia makubaliano na suala hilo huenda likaelekea mahakamani. Chama kimoja cha kuuza vito vya thamani kilisema kuwa bangili hiyo ni ya thamani ya dola 26,000 (sh milioni 57.2).

No comments

Powered by Blogger.