Header Ads

Meli za Oman kupeleka chakula Qatar



Baadhi ya makontena yaliyobeba vyakula katika bandari ya Oman
Baadhi ya makontena yenye chakula kutoka Oman, yakipakiwa kwenye meli kwa ajili ya kupelekwa Qatar.
DOHA- SERIKALI imefungua mpaka wake na Oman, kwa ajili ya kuruhusu huduma za usafiri wa meli kutoka nchini humo kwa lengo la kukabiliana na vikwazo vya usafiri vilivyowekwa na majirani.

Meli kadhaa zikiwa zimebeba vyakula na bidhaa mbalimbali, zimeonekana zikichukua uelekea wa kuja nchini kutokea bandari mbili zilizopo nchini humo. Qatar inategemea kwa asilimia kubwa uingizwaji wa chakula kutoka nje.
Saudi Arabia, Bahrain na Muungano wa Falme za Kiarabu, zilizuia uingizwaji wa bidhaa nchini wiki chache zilizopita kwa shutuma kuwa Qatar inaunga mkono vitendo vya kigaidi.
Waziri wa Mambo ya Nje nchini amewasili mjini London na kisha Paris kujadili mgogoro huo. Wakati hatua ya kuitenga Qatar ilianza wiki iliyopita, kulikuwa na ripoti za watu kununua chakula kwa wingi wakihofia kuwepo upungufu.
Lakini mwishoni mwa wiki, bidhaa kutoka Uturuki zilianza kuwasili katika maduka na ndege tano zilizosheheni matunda na mboga nazo ziliondoka nchini Iran. Meli tatu zilizosheheni tani 350 za chakula pia zinatarajiwa kuondoka nchini Iran kuelekea nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje anasema kuwa asilimia 16 ya chakula chake kilikuwa kinasafirishwa kupitia Saudi Arabia ambayo ilifunga mpaka wake.


No comments

Powered by Blogger.