Header Ads

Machinga wabuni mbinu mpya kuwaepuka askari wa jiji Nairobi



Hawkers sell their wares on Moi Avenue in Nairobi’s CBD on June 27, 2016 / MONICAH MWANGI
NAIROBI- WAFANYABIASHARA ndogo ndogo maarufu Machinga jijini hapa, wamebuni mbinu mpya ambayo inawawezesha kuepuka kukamatwa na askari wa jiji, katika harakati zao za kibiashara.

Mbinu hiyo ambayo imebainika kuwa ni kuja na watoto wao na kujifanya walemavu, imefanikiwa kuwaepusha na vipigo kutoka kwa askari wa jiji ambao wamekuwa wakiwakamata na kuwapeleka korokoroni kutokana na kufanya biashara kwenye sehemu zisizoruhusiwa.
Akizungumza na gazeti la The Star Kenya, mmoja wa ‘wamachinga’ hao amesema kuwa mbinu kubwa anayoitumia ni kuja na mtoto wake mchanga kwenye eneo ambalo anafanyia biashara ili asisumbuliwe na askari hao.
“Sijakamatwa kwa muda mrefu wala kuonewa na askari wa jiji, tangu nilipoanza kuja na mtoto wangu wa miaka miwili kazini hapa. Wakija wakinikuta na mtoto mdogo, basi wananiacha na kuondoka zao,” alisema Alice Mueni ambaye anafanya shughuli za biashara katika eneo la EastMatt Supermarket kwenye mtaa wa Tom Mboya.
Machinga mwingine ambaye alijitambulisha kama Michael Wambugu, alisema kwamba; “Hii ni wilaya yetu hivyo tunatakiwa kuishi hapa hapa. Wanataka sisi tuende wapi? Tutakuwa hapa muda wote la sivyo tutaanza kuiba.”
Hata hivyo, mbinu zao bado hazifui dafu kutokana na wamachinga hao kulazimika kuanza kazi nyakati za jioni ambazo zinakuwa hazina usumbufu wowote tofauti na mchana.

No comments

Powered by Blogger.