Header Ads

Korea Kaskazini yaituhumu Marekani



NEW YORK- KOREA Kaskazini imeituhumu Marekani kwamba, imeweka masharti magumu yasiyo ya haki kwenye ofa yake ya kutaka kufanya mazungumzo ya amani na taifa hilo.

Kupitia Balozi wake UN, Kim in Ryong, Korea Kaskazini iliwasilisha malalamiko hayo kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu masharti hayo ya Marekani.
Balozi Ryong alisema kwamba ni itakuwa ni ‘kosa kubwa la kimahesabu’ kwa mataifa au watu kuamini kwamba vikwazo vipya vilivyowekwa hivi karibuni vitaweza kuiziuia Korea Kaskazini kufanya majaribio ya makombora na silaha nyinginezo za kinyuklia.
“Vitendo vyao visivyo na busara wala maana, vinaweza kwenda kinyume na wao walivyotarajia kwani vikwazo vyao haviwezi kuizuia Korea Kaskazini kufanya majaribio ya silaha zake,”
“Marekani imekuwa ikisisitiza kuwepo kwa majadiliano hata sasa, lakini haileti maana kufanya majadiliano hayo ikiwa kuna masharti yasiyo ya haki yaliyoambatanishwa kwa ajili ya kutupa presha,” alisema Balozi Ryong kwenye mkutano maalum uliongozwa na Bolivia.
Marekani imekuwa ikisema kwamba, iko tayari kujadiliana na Korea Kaskazini lakini iwapo itasitisha mipango yake ya kufanyia majaribio makombora yake ya masafa na silaha za kinyuklia. Mwezi huu, baraza hilo la UN, liliweka vikwazo vipya 14 kwa taifa hilo ambalo limekuwa likikiuka maagizo ya Umoja wa Mataifa.

No comments

Powered by Blogger.