Header Ads

Barcelona kukipiga na Chapecoense Agosti 7



Image result for Chapecoense before plane crash
BARCELONA- UNAIKUMBUKA ile timu ya Chapecoense? Ngoja nikujuze kidogo, ni ile timu iliyopata ajali na kupoteza wachezaji wake 19 kwenye ajali ya ndege iliyotokea huko Medellin nchini Colombia.

Iko hivi, baada ya kuanza kushiriki tena ligi kuu ya kwao Brazil, sasa imepata mwaliko rasmi wa kucheza na timu ya Barcelona ya Hispania mnamo Agosti 7 mwaka huu kwenye dimba la Nou Camp.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Barcelona, mchezo huo unalenga kuirudishia morali timu na kuiwezesha kurejea kwenye levo za kimataifa za ushindani.
Mshindi wa mpambano huo, atatunikiwa tuzo maalum ambayo ni kombe la Joan Gamper.

No comments

Powered by Blogger.