Header Ads

Trump aunga mkono mpango wa nyuklia wa Iran



Rais Trump ameongeza makubaliano ya mpango wa kinyuklia kati ya Marekani na Iran
Rais wa Marekani, Donald Trump akizungumza na waandishi wa habari ikulu leo.
WASHINGTON DC, Marekani
IKULU ya Whitehouse nchini, imeendeleza mpango wa kuipunguzia vikwazo Iran licha ya Rais Donald Trump kuukosoa mpango huo.

Kuondolewa kwa vikwazo ni miongoni mwa makubaliano ya kinyuklia yalioafikiwa mwaka 2015, chini ya Rais mstaafu, Barrack Obama pamoja na mataifa mengine matano yenye uwezo mkubwa duniani.
Trump ameelezea makubaliano hayo kuwa mabaya zaidi. Hatahivyo, Wizara ya Fedha nchini iliwawekea vikwazo maofisa fulani na mfanyibiashara wa China anayehusishwa na mpango wa makombora wa Iran.
Hatua hiyo inamaanisha vikwazo vinavyozuia kampuni zozote za Marekani zinazoiuzia ama kushirikiana na Iran vitaendelea kulemazwa.
Kwa upande wake, Iran imekubali kupunguza mipango yake ya nyuklia, kupunguza uhifadhi wa madini ya Uranium, uzalishaji wa Plutonium na kuwaruhusu wachunguzi kuchunguza vifaa vyake.
Vikwazo vipya kutoka kwa Wizara ya Fedha vinaathiri watu binafsi wakiwemo maofisa wawili wa Iran, katika idara ya ulinzi na wanaouza makombora ya kijeshi ili kulipiza kisasi jaribio la kombora pamoja na hatua ya Iran kumuunga mkono, Bashar al-Assad wa Syria.
Raia wa Marekani na washirika wake sasa hawaruhusiwi kuingia mikataba na maofisa hao na kampuni husika.

No comments

Powered by Blogger.