Mchungaji aliwa na mamba akimwigiza Yesu
HARARE,
Zimbabwe
MCHUNGAJI
wa Kanisa la Saint of the Last Days,
Jonathan Mthetwa ameshambuliwa na kuliwa na mamba watatu wakati akionesha jinsi
Yesu alivyotembea juu ya maji.
Mthethwa
juzi alihamishia maombi yake kwenye eneo hilo ambalo linajulikana kama Mto wa
Mamba (Mto Mpumalanga), na kujaribu kuonesha kwa vitendo imani hiyo ya
kibiblia.
Kwa
mujbu wa mashuhuda, Mchungaji huyo aliingia majini na kujivuta umbali wa
takriban meta 30 kabla ya kujaribu kutoka nchi kavu. Bahati mbaya kwa Mchungaji
huyo, mamba watatu walimvamia na kumla.
Ni
makubadhi na nguo yake ya ndani pekee ndivyo vilivyopatikana, kwa mujibu wa
gazeti la The Daily Post la hapa.
Shuhuda
Deacon Nkosi alisema: “Mchungaji alitufundisha kuhusu imani Jumapili iliyopiya.
Aliahidi angetuonesha imani yake leo, lakini kwa bahati mbaya akaishia kufa
maji na kuliwa na mamba wakubwa watatu mbele yetu.
“Bado
hatuelewi kilichotokea, kwa sababu alifunga na kusali kwa wiki nzima.
Walimmaliza kwa dakika chache kabisa. Kilichosalia walipomaliza kumla ni jozi
ya makubadhi na nguo yake ya ndani ndivyo vilivyokuwa vikielea juu ya maji.”
Wakati
waokoaji wakiwasili eneo la tukio, tayari Mchungaji alishaliwa.
No comments