Mahakama ya Katiba kuamua hatima ya Zuma
Hatua
hiyo inajiri kufuatia hali ya sintofahamu kuhusu uongozi wa Zuma, huku kukiwa
na madai ya uajiri wa marafiki zake Serikalini na ufisadi.
Zuma
(pichani) hivi karibuni alizomewa katika baadhi ya mikutano ya hadhara huku maofisa
wakuu wa chama chake wakionekana hadharini kujipigia debe ili kumrithi kiongozi
huyo kama kiongozi wa chama.
Upinzani
unadai kwamba wabunge wanastahili kuongozwa imani yao na sio uongozi wa vyama
vyao, kwa kuwa uongozi wa rais Zuma ni suala muhimu la kitaifa.
Hatua
hiyo ya kupiga kura ya kutokuwa na imani naye ilisababishwa na kumfuta kazi Waziri
wa Fedha, Pravin Gordhan na naibu wake miezi miwili iliopita. Hatua hiyo
ilifanya uwezo wa kifedha wa taifa hilo kushuka.
Hata
hivyo, baadhi ya wachunguzi wanaamini kwamba hata iwapo Mahakama ya Katiba
itawapatia wabunge haki ya kupiga kura kwa siri, wanachama wengi wa ANC
watamuunga mkono kiongozi.
Kama
alivyosema mbunge mmoja, hataki kufuata wito wa upinzani na kwamba atakabili suala
la Zuma kama la ndani ya chama.
No comments