Keown: Wenger wauze Sanchez na Ozil
Mfaransa
huyo amesaini mkataba wa miaka miwili na amesema kuwa, timu yake inaweza
kupigana na kutwaa ubingwa msimu ujao. Viungo Alexis Sanchez na Mesut Ozil kwa
pamoja wanamaliza mikataba yao mwishoni mwa mwaka huu.
Keown
alisema kuliko kupata hasara ya kuwaruhusu kuondoka bure, ni vema akafanya
maamuzi magumu ya kuwauza nyota hao na kutengeneza faida itakayoweza kuleta
wachezaji wapya na wenye morali kubwa zaidi.
Sanchez
alifunga magoli 24 na kuchangia kupatikana kwa mengine 10, huku Ozil akifunga 8
na kuchangia 9 lakini yote hayo hayakutosha kuipa timu hiyo nafasi ya michuano
ya mabingwa wa Ulaya msimu ujao, jambo ambalo linatia ukakasi kwa Sanchez na
Ozil kuongeza mikataba yao.
Sanchez
amepewa ofa ya paundi 300,000 kwa wiki lakini bado hajasaini mkataba huo, huku
Ozil akikataa paundi 250,000 kwa wiki.
No comments