Aliyemuoa mwalimu wake aomba ndoa yao ivunjwe Marekani
Vili
Fualaau, ambaye sasa ana umri wa miaka 33, aliwasilisha nyaraka za kesi kwenye Mahakama
ya jimbo hili, akitaka ndoa yake ya miaka 12 na mkewe, Mary Kay Fualaau (zamani
akijulikana kama Letourneau), mwenye umri wa miaka 55 ivunjwe.
Fualaau
aliolewa akiwa na umri wa miaka 34 (akiwa na watoto wanne alipoanza uhusiano wa
kindoa na Vili Fualaau) baada ya kutumikia kifungo cha miaka saba na miezi sita
jela, wawili hao walioana kwa siri mnamo mwaka 2005.
Fualaau
aliwasilisha kesi ya kuachana nae mapema mwezi huu, bila kuelezea sababu ya
uamuzi wake huo. Katika ombi lake kwa mahakama, aliandika kwamba iwe yeye wala
mkewe hakuna aliye na mali wala mkopo.
Aidha,
Fualaau, ambaye ana watoto wawili na mkewe, alisema kwa sasa hawamtegemei tena,
akiomba wawili hao wagawanyiwe kile kidogo walichoweza kutafuta pamoja kwa
haki.
Hata
hivyo, mkewe hajatoa kauli yoyote kwa umma juu ya uamuzi wa mumewe. Fualaau
alikuwa darasa la sita alipoanza uhusiano wa kimapenzi mjini Seattle mwaka
1996.
Akiwa
mwalimu, Fualaau alikamatwa mwaka 1997 alipokuwa na mimba ya mtoto wao wa
kwanza, na baadaye alikiri kufanya kosa la ubakaji wa mtoto.
Hukumu
yake ya kwanza ya miezi sita ilipunguzwa baadae na kuwa ya miezi mitatu, chini
ya misingi kwamba angelikosa mawasiliano na mwanafunzi wake wa zamani. Lakini
katika kipindi cha wiki kadhaa wawili hao walikamatwa wakifanya ngono, na
akafungwa miaka saba.
No comments