Bintiye Mugabe ateuliwa bodi ya udhibiti vyombo vya habari Zimbabwe
Msemaji
wa Jeshi la Polisi nchini, Charity Charamba pia atahudumu katika bodi hiyo ya
watu 11 iliyoteuliwa na Waziri wa Mambo ya Ndani, Ignatious Chombo, pamoja na
wawakilishi wa makundi ya makanisa, wataalamu wa sheria na uhasibu na viongozi
wa kitamaduni.
Shirika
la kitaifa la habari limesema, bodi hiyo itadhibiti na kukagua vyombo vya
habari na sekta ya filamu nchini na kulenga ‘matumizi mabaya ya mitandao ya
kijamii wakati pia ikizingatia uchaguzi mkuu unaowadia mwaka ujao’.
Bona
amesoma nchini Singapore, na ana shahada ya uzamili katika masuala ya
usimamizi, hususan wa mabenki na fedha.
No comments