Header Ads

Trump aionya tena Korea Kaskazini



Meli ya Carl Vinson kwa sasa inaelekea rasi ya Korea 


Melivita ya Marekani iitwayo Carl Vinson ambayo iko njiani kuelekea katika eneo la rasi ya Korea, tayari kukabili vitisho vyovyote vya kivita vya Korea Kaskazini
WASHINGTON DC, Marekani
RAIS Donald Trump kwa mara nyingine ameionya Korea Kaskazini kupitia mtandao wa twitter, kwa kusema kuwa taifa hilo linatafuta matatizo.

Aidha, Trump alilitaka taifa la China ambalo ni mshirika mkuu wa Korea Kaskazini kujaribu kukabiliana na jirani wake huyo.
Trump alipendekeza kuwa China itapata makubaliano bora ya kibiashara ikiwa itafanya hivyo, lakini akaongeza kuwa Marekani haitaogopa kutatua tatizo la Korea Kaskazini pasipo uwepo wa China.
Trump alitoa matamshi kama hayo wiki moja iliyopita, lakini tangu wakati huo msukosuko umekuwa mkubwa. Marekani imetuma meli za kivita kuenda kwa maji ya rasi ya Korea, hatua ambayo imechochea ghadhabu ya Korea Kaskazini.
BBC

No comments

Powered by Blogger.